KWA WEWE UNAYEPENDA KUPIKA TUUNGANE HAPA


Ikiwa leo ni Jumapili nzuri ya Disemba 26 mwezi wa Januari habarimkusanyiko.blogspot.com inapenda kukukaribisha 'Jikoni Kwetu' ili tuweze angalau kupika mwishoni mwa weekend hii.


Na leo tutakwenda kuangalia namna ya kupika  pishi la la choroko na tunaanza namna hii Karibu!!

MAHITAJI
Choroko kikombe 1 na nusu

Nyanya 1/2 kopo

Swaum kijiko kimoja cha chai

Kitunguu kikubwa 1

Curry powder 1 kijiko cha chai

Chumvi kiasi

Nazi kopo 1

Olive oil

Pilipili nzima

NAMNA YA MATAYARISHO

Unapotaka kupika pishi hili ni vizuri uwe umejipanga siku moja kabla maana ni vizuri ukaloweka choroko usiku mzima kisha siku inayofuata utazichemshe choroko zako hadi ziive kisha baada ya kuiva utaziweke pembeni.

Baada ya hatua hiyo utasaga nyanya zako na kuandaa kitunguu pamoja na swaum kisha utavipika mpaka kiasi, baada ya hapo tia mafuta na curry powder, pika mpaka nyanya zitoe mafuta kisha tia choroko, tui la nazi, maji nusu kikombe, pilipili na chumvi, kisha koroga vizuri na uache ichemke.

Pika mpaka tui la nazi litakapoiva na rojo ibakie kidogo sana, kisha ipua na mboga yako itakuwa tayari kwa kuliwa. Unaweza kula mboga hii kwa wali, ugali na wakati mwingine hata kwa chapati inaenda pia. Asante.


Pishi hili maalum kwa ajili ya weekend yako limeandaliwa na kuletwa kwenu na Asha Habibu.

No comments:

Post a Comment

Ad Inside Post

Comments system

Disqus Shortname