WANAFUNZI WAWAUMBUA MADAKTARI BAADA YA KUSINZIA KAZINI


Tatizo la uhaba wa wataalam wa afya wakiwemo madaktari ni moja ya tatizo linaloyakabili mataifa mengi ya Afrika na Marekani Kusini , jambo linalowalazimu madaktari na wauguzi kufanya kazi ya ziada ilikuwatunza wagonjwa.


Imekuwa ni kawaida sana kumsikia daktari anayehudumu katika hospitali ya umma ndiye yuleyule anayekimbia kumhudumia mgonjwa katika hospital ya kibinafsi iliapate pesa za ziada.

Tumekuwa tukisikia taarifa mbalimbali kuhusu madaktari kufanya makosa ndani ya chumba cha upasuaji na hata mara nyingine katika vyumba vya wagonjwa mahututi kwa sababu ya uchovu.

Huko nchini Mexico wagonjwa na jamaa zao wameanzisha kampeini ya kuwatetea wanafunzi wanaojifunza kazi. Ambao wao waliamua kuwapiga picha madaktari wakisinzia na kuzichapisha katika mitandao ya kijamii.
Daktari akiwa kasinzia kazini
''inakuaje daktari ambaye anawajibu wa kuwatunza wagonjwa 12 anasinzia kazini ''Hii ni kama rubani kusinzia ndege ikiwa angani '' alisema mwandishi wa blogu aliyechapisha picha hizo.

Watu waliochangia mjadala huo katika mitandao ya kijamii walidai kuwa madaktari wakuu wamekwenda kulala na kuwaachia wanafunzi wao kazi nyingi.

Huyu daktari naye hana habari kabisa
Hata hivyo, baada ya mjadala huo katika vyombo vya habari ilibainika kuwa madaktari hao hufanya kazi wakati mwingine hata zaidi ya saa 36 bila mapumziko.

Mbali na hayo, wengi waliwashtumu madaktari waliohitimu wakisema kuwa wanawatelekeza wagonjwa wao kufuatia kuimarika maradufu kwa mishahara yao.

No comments:

Post a Comment

Ad Inside Post

Comments system

Disqus Shortname