Askofu Mkuu Mstaafu wa Cape Town, Desmond Tutu,
amelazimika kuahirisha mipango ya ziara zake kwa mwaka mzima ujao kutokana na
sababu za kiafya.
Taarifa iliyotolewa na taasisi yake imeeleza kuwa Askofu huyo anakabiliwa na
tatizo la tezi dume ambayo ameshadumu nayo miaka kumi na mitano iliyopita, na
hivyo ataanza matibabu hivi karibuni ili kukabiliana na tatizo hilo.
|
Askofu Desmond Tutu |
Mbali na hayo habari ziliendelea kusema kuwa, binti wa Askofu huyo
amemuelezea baba yake mwenye umri wa miaka themanini na miwili, kwamba
hatahudhuria tuzo za Nobel zitakazo fanyika baadaye wiki hii huko Rome, Italia.
Ni vizuri ukamshirikisha ndugu, jamaa, na hata rafiki pia kuhusu uwepo wa blog hii ya habarimkusanyiko.blogspot.com, tambua ya kuwa tunathamini sana mchango wako wewe msomaji wetu na tunakusihi endelea kuwa nasi siku zote
No comments:
Post a Comment