JITIHADA ZA KUTAFUTA NDEGE ILIYOPOTEA ZAANZA KUZAA MATUNDA, MIILI 40 IMEOPOLEWA BAHARINI



Maafisa usalama wakiwa katika harakati za utafutaji wa ndege
Kufuatia kupotea kwa ndege ya shirika la ndege la Asia ndege namba QZ8501At ,miili arobaini imeopolewa kutoka baharini katika utafutaji wa mabaki ya ndege hiyo na utafutaji unaendelea.

Miili hiyo ilionekana ikielelea karibu na taka za bahari pwani ya Indonesia,eneo la Borneo moja ya eneo la utafutaji mabaki ya ndege hiyo.Na taarifa kutoka serikali ya Indonesia zimethibitisha kwamba miili hiyo inatoka katika ndege iliyopotea.

Ndege hiyo aina ya Airbus A320-200,ilikuwa imebeba abiria 162 ikitokea Surabaya nchini Indonesia kuelekea Singapore, ilipotea siku ya Jumapili.

Utafutaji wa mabaki ya ndege hiyo umeingia katika siku ya tatu,na eneo la utafutaji limeongezwa na kufikia kanda kumi na tatu hii inashirikisha nchi kavu na baharini.

Taarifa zinasema kuwa, wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliooneshwa wazi kwenye runinga ya taifa la Indonesia picha za taka bahari zilioneshwa zikiwa zimechanganyika na mabaki ya miili ya abiria ikielea majini.

Ndugu wa mabaki hayo walipoona picha hizo walikubwa na fadhaa kuu na walionekana kushtushwa na picha hizo. Baadaye askari wa majini nchini Indonesia wameeleza kuwa miili hiyo arobaini iliopolewa na meli ya kivita.

Mkurugenzi mtendaji wa AirAsia Fernandes ali ingia katika mtandao wa twitter na kueleza huzuni yake kwa ndugu waliopoteza ndugu zao katika ndege QZ 8501. Na kwa niaba ya shirika la ndege la AirAsia ametuma salamu za rambi rambi .
Hata hivyo, utafutaji wa miili na mabaki ya ndege hiyo unaendelea na unashirikisha meli thelathini, ndege kumi na tano na chopa saba.

Ni haki yako kupata kila habari inayotufikia, asante sana kwa kutembelea habarimkusanyiko.blogspot.com
Source: BBC

No comments:

Post a Comment

Ad Inside Post

Comments system

Disqus Shortname