WAMACHINGA NA OMBAOMBA WATAFUTIWA DAWA YAO DAR


Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadiki

Jiji la Dar es Salaam linaangalia upya uwezekano na utaratibu wa kuwaondoa ombaomba na wafanyabiashara ndogondogo (wamachinga)  katika maeneo yasiyoruhusiwa katika jiji hilo, baada ya sheria na hatua zinazochukuliwa ikiwemo kuwarudisha ombaomba hao katika mikoa wanayotoka kuonekana kugonga mwamba na tatizo hilo kuonekana kuendelea kuwa sugu kufuatia wengi wao kurudi katika maeneo ya awali kila wanapoondolewa.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecki Sadiki wakati alipokuwa akifuangua kikao cha wajumbe wa Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Dar es Salaam (RCC) kilichofanyika Desemba 17 jijini Dar es Salaam kujadili masuala mbalimbali ya mendeleo katika jiji hilo.

 Sadiki, alisema kuwa kuendelea  kuwepo kwa wafanyabiashara hao katika maeneo yasiyo rasmi ni moja ya changamoto inayolikabili jiji la Dar es Salaam kutokana na biashara wanazozifanya kuchangia kuzuia maeneo ya barabara ya waenda kwa miguu, kusababisha uchafuzi wa mazingira, kusabisha msongamano wa magari kwa baadhi yao kuweka bidhaa  barabarani.

Aidha, Sadiki aliendelea kusema kwamba, kutokana na hali hiyo baadhi ya wafanyabiashara walio na biashara rasmi  ambao hulipa kodi za Serikali wamekuwa wakilalamikia hali  ya ukwepaji wa kodi inayofanywa na wafanyabiashara hao.
Wafanyabiashara wadogo wadogo (wamachinga) wakiwa wamepanga bidhaa zao kandokando ya barabara ya Kawawa jijini Dar es Salaam

Wamachinga wakiendelea na biashara zao eneo la Karume jijini Dar es Salaam
 
Mzee mwenye uwezo duni akiwa anaomba wapita njia

Mmoja wa wazee wanaoomba akijaribu kuomba kwa wapita njia

 Mbali na hayo, Sadiki aliongeza kuwa  mpango wa mkoa wa sasa ni kuendelea kuwatumia wafanyabiashara hao kama  fursa ya mtaji wa rasilimali watu ambayo itatumika kama chanzo cha mapato katika kuleta maendeleo ya mkoa.

Lengo la habarimkusanyiko.blogspot.com ni kuhakikisha unapata habari mbalimbali kutoka kwetu, asante kwa kuwa nasi

No comments:

Post a Comment

Ad Inside Post

Comments system

Disqus Shortname