Showing posts with label Wanyama. Show all posts
Showing posts with label Wanyama. Show all posts

FAHAMU MAMBO MUHIMU AMBAYO HUKUWAHI KUYAJUA KUHUSU MNYAMA PUNDAMILIA



Na, Shadrack D. Daniel
Habarimkusanyiko.blogspot.com kuanzia sasa itakuwa ikikuletea mambo mbalimbali kuhusu wanyama wa porini kuanzia tabia zao pamoja na namna ambavyo wanaishi katika mazingira yao na leo kwa kuanza tunaanza na myama anayeitwa Pundamilia.

Pundamilia ni wanyama ambaye yupo katika familia ya wanyama ijulikanayo kama “equids” mnyama huyu hufahamika sana kutokana na kuwa na rangi yao ya michirizi myeupe na myeusi.

Na kitu cha kushangaza zaidi ambacho naamini wengi wetu tulikuwa hatukijui ni kwamba michirizi ya wanyama hawa huwa na mipangilio tofauti kwa kila pundamilia.

Kingine cha ajabu na cha kushangaza zaidi ni kuwa michirizi ya wanyama hawa hutumika kwa ajili ya kumsaidia kujificha na kujihami na mazingira yao, lakini pia michirizi hiyo humsaidia mtoto wa pundamilia kumtambua mama yake katika kundi la takribani pundamilia 15 .

Kama ilivyo kwa viumbe vingine na hata wanyama hawa jike hukua kwa haraka zaidi kuliko dume, lakini pia pundamilia jike huweza kupata mtoto akiwa na umri wa miaka kuanzia mitatu na mtoto ni moja kwa kipindi cha miezi 12 , huku akibeba mtoto tumboni kwa kipindi cha mwaka moja.

Pundamilia ni wanyama walao nyasi pia pundamilia dume huwa na uzito mkubwa kuliko jike na hukaliliwa kufika taribani kilo 320.

Ni haki yako kuyapata yote hayo, tafadhali endelea kutupa nafasi tukujuze mengi zaidi

Ad Inside Post

Comments system

Disqus Shortname