Showing posts with label arusha. Show all posts
Showing posts with label arusha. Show all posts

VIJANA WASHAURIWA KUACHA KUTEGEMEA KUAJIRIWA




 Arusha, Theo.M.George 
Vijana vya vyuo vikuu vya Jumuiya ya Afrika mashariki washauriwa kuachana na mitazamo potofu kwa kuitegemea serikali kuwaajiri na badala yake wanapaswa kuangalia njia mbadala yakuweza kujiajiri wao wenyewe kwa kuanzisha miradi mbalimbali itakayo wasaidia kujiendeleza kimaisha.

Hayo yalisemwa na Katibu wa Wizara ya vijana kutoka Kigali nchini Rwanda, Rosemary Mbabazi katika mkutano wa vijana wa Afrika Mashariki ulioanza Disemba 5 mwaka huu katika ukumbi wa mikutano ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) jijini Arusha.

Mbabazi alisema kuwa, vijana wengi wamekuwa wakiitegemea serikali kuwapatia ajira mara tu baada ya kumaliza masomo yao, jambo linapelekea vijana wengi kuishia kuilaumu serikali pindi wanapokosa nafasi hizo za ajira na hatimaye wengine kukata tamaa kabisa.

Mkutano huo uliojumuisha viongozi mbalimbali wa kutoka nchi za jumuiya ya Afrika Mashariki na wanafunzi wa vyuo vya Afrika Mashariki ulinuia kutoa elimu kwa vijana jinsi ya kutatua matatizo yanayo wakabili, pamoja na namna ya kukabiliana na changamoto za kimaisha katika maisha yao kila siku.

Naye afisa mkuu Prof Nuhu Hatibu wa Kilimo Trust kutoka Kampala nchini Uganda alisema kwamba "baadhi ya changamoto zinazo wakabili vijana ni kujiingiza katika matumizi ya madawa ya kulevya na kuwepo kwa ongezeko kubwa la virusi vya Ukimwi,(HIV/AIDS) jambo linaloathiri vijana kwa kiasi kikubwa katika nchi za jumuiya ya Afrika Mashariki"

Afisa huyo aliongeza kusema kuwa, vijana wanatakiwa kutambua kuwa kilimo ni moja ya njia ambayo inaweza kuwakwamua kiuchumi kwa kufuata taratibu za kilim,  ikiwa ni pamoja na vitendea kazi kama upatikanaji wa trekta ,plau, sambamba na mbolea itakayo saidia katika kilimo

Sambambana na hayo mkutano huo iliongozwa na  kaulimbiu isemayo  "Kijana. fikiria,Ongea na Shiriki (Youth.Think,Speak,Participate)’’

Unastahili kupata habari zote hizi kila kona ya Tanzania, tafadhali endelea kuungana nasi kila. siku 

WATANZANIA WATAKIWA KUCHAGUA VIONGOZI BORA



 Arusha, Na Theo M George.

Watanzania wametakiwa kuwa makini na viongozi wanao wachagua kuongoza wananchi kwa kuangalia vigezo vya utendaji kazi kwa maslahi ya wananchi na sio ushabiki wa kivyama.

Hayo yamesemwa jana na Diwani wa kata ya Elerai Jeremiah Mpinga wakati wa kumnadi mgombea Jonas Bethuel Temba kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo( CHADEMA) katika kampeni zinazo endelea jijini Arusha za kuwachagua wenyekiti wa mitaa.

Mpinga aliesema kuwa, wananchi wanapaswa kutambua kuwa kiongozi bora ni yule anayejali na kutetea haki za wanyonge na taifa kwa ujumla kwa kuboresha miundo mbinu na kwa kuzingatia huduma bora za kijamii ikiwemo huduma za afya, kiuchumi na kufuata demokrasia iliyo na maslahi kwa taifa na sio kwa manufaa ya chama.

Aidha, aliongeza kuwa, taifa linahitaji viongozi waadilifu na kusisitiza kuwa endapo mgombea atachaguliwa na wananchi na atashindwa kutekeleza aliyo yaahidi wakati wa kampeni zake uongozi na wananchi watachukua jukumu la kumuondoa madarakani kama ilivyofanyika kwa baadhi ya viongozi wa chama hicho  katika mitaa mbalimali ambao walichaguliwa kupitia chama hicho.

Naye mgombea Jonasi Bethuel Temba, amewasisitiza wananchi kumpigia kura na kuwataka wajitokeze kwa wingi  mara ifikapo Desemba 14, 2014, ili taifa liweze kupata viongozi bora watakao liongoza taifa kwa misingi ya kidemokrasia na maslahi ya taifa kwa ujumla.




Unastahili kupata taarifa zote kutoka hapa nchini kupita habarimkusanyiko.blogspot.com, asante kwa kuendelea kutuunga mkono

Ad Inside Post

Comments system

Disqus Shortname