TCRA YAFUNGA VITUO VYA TV NA REDIO KWA MAKOSA YA KUKWEPA KODI

Mamlaka ya Mawasiliano TCRA imevifungia vituo 21 vya Radio na 6 vya TV kikiwemo kituo chaStar TV, Radio free Afrika, Kiss Fm na Uhuru FM kwa kushindwa kulipa kodi ya lesseni kwa wakati .

Akitangaza uamuzi huo, mkurugenzi wa habari na mawasiliano wa TCRA Innocent Mungy, amesema kuwa mitambo ya vituo hivyo itazimwa ifikapo kesho Januari 17 saa 6 usiku, na itawashwa baada ya vituo hivyo kulipa madeni yanayowakabili na endapo kituo chochote kitakaidi basi kitachukuliwa hatua kali za sheria.

SERIKALI YAITAKA TBC KUJIENDESHA KIBIASHARA


Shirika la Utangazaji la Tanzania (TBC) limetakiwa kujiendesha kibiashara na kufanya shughuli zake kwa kuzingatia maadili ili liwe shirika linalofanya kazi vizuri na kutimiza wajibu wake.

Hayo yalisemwa na Waziri wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye wakati alipokutana na Bodi ya Wakurugenzi ya TBC, Dar es Salaam jana.

WAZIRI MKUU MAJALIWA NAYE KAFIKA KUMJULIA HALI SUMAYE

12541064_10153842809569339_6210438068788157892_n
Magazeti mengi ya Januari 12, 2016 yaliripoti kuhusu Rais Magufuli kuamua kumjulia hali Waziri Mkuu Mstaafu Frederick Sumaye katika Hospitali ya Muhimbili.

MAALIM SEIF ASEMA HATAMBUI KUHUSU KURUDIWA KWA UCHAGUZI WA ZNZ NA HAWATAKUBALI

Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi (CUF) na aliyekuwa mgombea urais wa Serikali ya
Mapinduzi Zanzibar  Maalim Seif Sharif Hamad amesema kuwa hana taarifa zozote juu ya swala la kurudiwa kwa uchaguzi na badala yake amehitaji kura zilizobaki zihesabiwe na mshindi aweze kutangazwa.

Akizungumza leo na waandishi wa habari katika hotel ya Serena jijini Dar es Salaam, Maalim Seif amesisitiza kuwa hoja ya kurudia uchaguzi wa Zanzibar kama inavyoelezwa na viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), haina msingi, haikubaliki na sio halali kikatiba.

SAMMATA AENDELEA KUPOKEA PONGEZI ZAKE AWAMU HII NI KUTOKA KWA JK


Baada ya Mbwana Samatta kufanikiwa kushinda Tuzo ya mwanasoka Bora wa Afrika kwa Wachezaji wa ndani, Rais Mstaafu wa awamu ya nne Mhe Jakaya Mrisho Kikwete naye ameonana na mchezaji huyo na kumpongeza kufuatia kutwaa tuzo hiyo.

RAIS MAGUFULI KAMTEMBELEA WAZIRI MKUU MSTAAFU FREDERICK SUMAYE HOSPITALINI


Kumekuwa na ripoti mfululizo kwenye vyombo vya habari kuhusu kuumwa na kulazwa kwa Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye katika hospitali ya Muhimbili huku kukiwa hakuna ripoti inayotaarifu ugonjwa wake.

WASTARA KAYASEMA HAYA BAADA YA KUFANIKIWA KUFUNGA NDOA NA MBUNGE



WASTARA X
Hivi karibuni kulikuwa na tetesi zilizokuwa zikimuhusu muigizaji Wastara kufunga ndoa na mtu aliyetajwa kuwa ni Mbunge.

Hatimaye tetesi hizo zimekata baada ya kubainika kuwa ni kweli muigizaji huyo kafunga ndoa na Mbunge wa Jimbo la Donge Zanzibar, Sadifa Khamis Juma. ambaye pia ni Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa chama cha CCM (UVCCM).

ZIFAHAMU SABABU AMBAZO HUZUIA VIJANA WENGI KUTOFANIKIWA KATIKA MAISHA

Ikiwa tayari tumeingia ndani ya mwaka mpya 2016 na kila mtu tayari anayo mipango mipya na malengo ndani ya mwaka huu.

Lakini mipango yetu ya kimafanikio mara nyingi hurudishwa nyuma kutokana na fikra zetu wenyewe na kujikuta wengi tukiishia kulalama wenyewe au kuwalaumu watu wetu wa karibu na kuwaona kama ndio chanzo cha kurudisha nyuma mafanikio yetu.

PICHA RASMI YA RAIS MAGUFULI TAYARI IMETOKA IPO HAPA

Picha rasmi ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh John Pombe Magufuli imeshatoka katika ofisi ya idara ya habari maelezo jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo Bi Zamaradi Kawawa kuwa picha hiyo itauzwa kwa shilingi 15,000 ya kitanzania bila ya kuwekwa fremu, huku picha ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere itauzwa kwa shilingi 5000/=

MILIONI 6 ZA G. NAKO ZAPOTEA KWENYE KIKAO CHA WASANII!!

Mkali wa muziki wa kizazi kipya kupitia crew ya Weusi G.Nako amejikuta akiuanza mwaka 2016 vibaya baada ya kupoteza pesa nyingi zipatazo dola 3,000 alipokuwa kwenye kikao cha wasanii.

Hayo yamebainika kupitia U Heard ya Januarii 07, 2016 inayofanywa na Soudy Brown kupitia show ya XXL ya Clouds Fm.

HAYA NDIO MAAMUZI MENGINE YA MHESHIMIWA KINGWANGALA



Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla ameagiza Watanzania wote kutokubali kutozwa rushwa kwa ajili ya damu salama na baadala yake kwa mtu atakayefanya hivyo atachukulia hatua kali za kisheria.


Kauli hiyo imetolewa na Dkt. Kingwangalla alipofanya ziara katika Ofisi za Mpango wa Taifa wa Damu Salama zilizopo jijini Dares Salaam.

HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI YAPATA CT SCAN MPYAA

Hatimaye agizo la Rais Dkt. John Pombe Magufuli la kupatikana kwa mashine mpya ya CT Scan katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili limeonekana kuzaa matunda baada ya Serikali kununua mashine mpya ambayo imegharimu zaidi ya bilioni 3.6 kwa pesa ya Kitanzania.

Kutokana na mashine zilizokuwepo mara ya kwanza kuharibika kila wakati Serikali imegharamia mashine mpya ambayo imeelezwa kuwa na uwezo mkubwa wa kufanya kazi tofauti na nyingine zilizowahi kutumiwa na hospitali hiyo.

WAZIRI MWIGULU NCHEMBA KAYAAMUA HAYA KWA WATUMISHI WABADHIRIFU MKOANI PWANI















Waziri wa Kilimo Mifugo na Uvuvi,Mh.Mwigulu Lameck Nchemba leo amefanya ziara nyingine mkoa wa Pwani na kutoa maamuzi ya kuwasimamisha kazi watumishi wengine kwa tuhuma za ubadhirifu pamoja na kuamua kuzuia malipo ya mshauri wa ujenzi wa machinjio ya kisasa iliyopo Ruvu mkoa wa Pwani.

Mbali na hayo, Waziri huyo ameagiza wajumbe wa bodi hiyo inayosimamia ujenzi wa machinjio hiyo kuvunjwa siku ya Jumatano January 6, 2016 kwa tuhuma za matumizi mabaya ya pesa.

KAMA UNAPENDA KUISHI NA FURAHA MWAKA HUU 2016 FANYA MAMBO HAYA MATANO MUHIMU

Ikiwa leo ni Januari 04, 2016 mwaka ndio kwanza unaanza kabisa nimeona ni vyema tufahamishane haya mambo ya msingi yatakayokusaidia kuishi ukiwa na furaha ndani ya mwaka huu.


Kuna baadhi ya watu wamekuwa wakiishi pasipo kuwa na furaha kwa muda mrefu kutokana na sababu za kimaisha pamoja na magumu wanayoyapitia katika mazingira yao ya kila siku.

Ad Inside Post

Comments system

Disqus Shortname